Kitabu hiki kinahusu biashara na kinatoa mwongozo kwa watu wenye ndoto za kuanzisha biashara. Msomaji atajifunza jinsi ya kuanzisha, kuendeleza na kusimamia biashara yake kwa ufanisi na kupata faida nzuri kupitia biashara yake. Kitabu hiki kinatoa mafunzo ya Biblia juu ya biashara na mifano 24 ya biashara tofauti tofauti, changamoto pamoja na faida zake. Pia kinatoa fursa kwa msomaji kujifunza namna ya kufanikiwa kutoka kwa Nabii Mkuu Mhe. Dkt. GeorDavie ambaye amefanikiwa sana katika nyanja zote; kimwili, kiroho na kiuchumi. Hivyo kitabu hiki ni muhimu kwa mtu yeyote mwenye ndoto ya kuanzisha/kupanua biashara na kufanikiwa kiuchumi.